Dkt. Pindi Chana na RC Mongela wakutana na Kamati ya Maandalizi ya Mkutano wa kimataifa wa UNWTO

Zikiwa zimebaki takribani siku mbili kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Kimataifa wa 65 wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani Kanda ya Afrika (UNWTO) – CAF, utakaofanyika jijini Arusha Oktoba 5 hadi 7, 2022, Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Dkt. Pindi Chana na Mkuu wa mkoa wa Arusha John Mongela pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Arusha leo Oktoba 3, 2022 wamekutana na Kamati ya maandalizi ya Mkutano huo ya Wizara ya Maliasili na Utalii ili kupokea taarifa ya maandalizi ya mkutano huo utakaofunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Likes:
0 0
Views:
397
Article Tags:
Article Categories:
Tourism