Mlima Bulera: Sehemu iliyokuwa na visima vya ajabu kwenye  mawe

Mlima Mwalolera au kama unavyofahamika pia kama Mlima Bulera unapatikana katika maeneo yenye uoto wa asili katika mkoa wa Geita.

Mt. Bulera: A mountain full of history as you climb each step. It is on this mountain that you get to see the footprints of Mwanamalundi the famous Sukuma traditional healer and a witch.
On the sides of the mountain, there are huge rocks with holes poked for rituals, as well as holes for the (Bao game) for entertainment. Currently, this area is used by residents for various activities such as agriculture and livestock keeping.

Hapa kuna alama mbalimbali za kihistoria vikiwemo visima vitatu vilivyokuwa kwenye miamba ya mawe katika mlima huu, ambapo visima hivyo vilitumika kama vyanzo vikuu vya maji kwa wakazi wa jirani na mlima huu.

Visima hivyo vilikuwa na maajabu yake kwani ilikuwa ni mwiko kwa mtu mwenye kitovu kikubwa kusogelea, pia ilitakiwa kusogea maeneo hayo ukiwa peku, na mama mwenye watoto pacha hakutakiwa kabisa maeneo hayo.