UTALII WA KUVUA SAMAKI

Utalii wa kuvua samaki ni mchezo wa kukamata samaki ndani ya maji na kuwatoa nje kisha kuwarudisha tena majini bila kuwadhuru.

Mchezo huu hufanywa na mtalii ambaye huendeshwa kwa kutumia boti na hupewa ndoano ili avue samaki na baada ya kumpata hupiga picha na samaki ili kuthibitisha kama amevua kisha kumrejesha majini.

Watalii wakiwa wengi ndani ya boti moja ndiyo mchezo hunoga zaidi kwani hushindana nani mwenye bahati ya kuvua samaki hivyo huleta amani, upendo na umoja baina ya watu.

Utalii huu upo mkoani Iringa wilayani Mufindi katika kijiji cha Luhunga.

Likes:
0 0
Views:
721
Article Categories:
Uncategorized