Kanisa la kilutheri lenye miaka 112  mkoani Njombe

Kanisa la kilutheri Lupembe lilijengwa na wajerumani mwaka 1903 na kufunguliwa rasmi mwaka 1911 mkoani Njombe.

Wakati wa ujenzi wa kanisa hili  wazawa chini ya Chifu Lupembe Hongoli walitumika kama nguvu kazi ambapo walikuwa wanalazimishwa  kusomba maji kwa kichwa kutoka mtoni ,kukusanya mawe,kufyatua matofali  ,pamoja na kupasua mbao kutoka katika misitu ya iditima  ambayo mpaka sasa inamilikiwa na wakala wa misitu Tanzania.

Baada ya vita vya kwanza kati ya waingereza na wajerumani  jengo hili halikutumika tena kwa ajili ya ibada bali lilitumika, kwaajili ya kuhifadhia silaha za kivita.

Mpaka sasa kanisa hili linaendelea kuhifadhi historia yake ikiwa pamoja na mabaki ya silaha za zamani zilizokuwa zinatumiwa na Muingereza katika vita vya kwanza vya dunia.

Likes:
0 0
Views:
762
Article Categories:
History